Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kimataifa. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kimataifa. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 13 Aprili 2017

Wayne Rooney Kuondoka Man Utd Mwisho wa Msimu

Nahodha wa Manchester United, Wayne Rooney.

Nahodha wa Manchester United, Wayne Rooney ataondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Mmoja wa wachezaji wa timu hiyo ndiye aliyevujisha siri, kwamba Rooney hana raha na anaona ni wakati mwafaka kwake kuondoka Old Trafford kwa kuwa hapati nafasi ya kucheza.

Kocha Jose Mourinho anaonyesha kutomuweka Rooney kama chaguo la kwanza lakini mara kadhaa, naye amekuwa akiumia.

Rooney ambaye amecheza Man United kwa miaka 13 tokea alipojiunga nayo akiwa kinda kutoka Everton, amekuwa akiandamwa na mamumivu ambayo pia yamechangia akose mechi kadhaa.

Imeelezwa, hana uhakika pia kucheza mechi ijayo ya Man United ambayo itakuwa ya Europa League dhidi ya Anderlecht na itapigwa nchini Ubelgiji, Ahamisi.

Jumanne, 9 Februari 2016

Liverpool 'OUT' Michuano ya FA

ImageGettyImageRaha ya mechi bao, wachezaji wa West Ham United wakishangilia

Wagonga nyundo wa London West Ham United imewatupa nje majogoo wa Anfield Liverpool katika mchezo wa raundi ya nne ya kombe la FA.

West Ham walianza kuandika bao lao la kwanza kupitia kwa Michail Antonio katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza baada ya kunganisha krosi nzuri Enner Valencia's

Liverpool wakachomoa bao hilo kupitia kwa kiungo Philippe Coutinho aliyepiga mpira wa adhabu na kujaa nyavuni moja kwa moja.

ImageGettyImageWest Ham sasa watakutana na Blackburn raundi ijayo

Dakika tisini zikamalizika kwa sare ya bao 1-1, katika dakika 30, za nyongeza West Ham wakapata bao kupita kwa Angelo Ogbonna,

West Ham watawavaa Blackburn ugenini katika mchezo wa raundi ya tano ya michuano hiyo hapo Februari 21.

Jumatatu, 8 Februari 2016

Wenger:Arsenal Itaichakaza Leicester Jumapili

JUMAPILI

By Meshack Brighton

19:24ENGLISH FOOTBALLSHARE

0

Getty

Arsene Wenger anaamini Arsenal yake ina uwezo wa kutosha kuwapiga vinara wa Ligi Kuu Leicester City Jumapili ijayo

Washika mtutu wa London wapo nafasi ya pili katika msimamo wa ligi baada ya ushindi mwepesi dhidi ya Bournemouth. Magoli kutoka kwa Mesut Ozil na Alex Oxlade-Chamberlain yaliyopishana kwa muda wa sekunde 88 – kuhitimisha mwenda wa Arsenal wa saa tano na nusu bila ya goli.

 “[Kuifunga Bournemouth] ni vizuri sana kwa ajili ya mustakabali kwani sasa tuna mechi kubwa nyumbani dhidi ya Leicester ambao wana nafasi kubwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu,” Wenger alikiambia Arsenal.com. “Ushindi kwa namna Fulani unakuweka katika hali nzuri kwa ajili ya mchezo unaofuata.

“Tuna wiki moja ya kujiandaa na mchezo huo na ninautafakari sana. Leicester ni timu imara lakini nasi tupo imara pia. Nyumbani tukiwa na mashabiki wetu tutawafunga tu.”

Mfaransa huyo aliwamwagia misifa Chamberlain na Gabriel kwa kushiriki kuwezesha ushindi kupatikana Jumapili.

 “Oxlade-Chamberlain ana nguvu, mbinu na mwenye uwezo wa kufunga magoli lakini anaweza kutengeneza nafasi pia,” aliongeza Wenger. “Mara nyingi hana bahati [na mashuti yake] lakini nadhani hilo litamshawishi kujaribu Zaidi na Zaidi.

“Gabriel amefanya vizuri. Ameonyesha kiwango safi na kwa ujumla nadhani anazidi kujiamini kadiri anavyocheza mechi nyingi, jambo linalofurahisha.”

 

Zouma Kukaa Nje Miezi 6

ImageReuters

Beki wa klabu ya Chelsea Kurt Zouma atakua nje ya uwanja kwa miezi sita baada ya kuumia goti kwenye mchezo dhidi ya Manchester United.

Zouma, atafanyiwa upasuaji kwenye kwenye goti lake ambalo aliumia Jumapili uwanjani Stamford Bridge baada ya kutua vibaya aliporuka kupiga mpira kwa kichwa.

Uchunguzi umethibitisha kwamba aliumia vibaya na hivyo anapaswa kufanyiwa upasuaji kutibu tatizo hilo.

Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL

Kawaida, Mchezaji akipata majeruhi ya aina hii, basi huwa nje ya uwanja si chini ya Miezi hivyo mchezaji huyu atakosa michezo yote ya msimu uliobaki.

ImageReutersImageZouma alionekana kuhisi uchungu mwingi baada ya kuanguka

Zouma, ambaye amekuwa kama pacha wa John Terry uwanjani, ameichezea Chelsea mechi 32 msimu huu.

Ameshaichezea Ufaransa mechi 2 za Kimataifa.

Cristiano Ronaldo:Nataka kubaki RealMadrid

ImageGettyImageCristiano Ronaldo

Nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amesema hataki kuondoka klabuni hapo kabla ya mkataba wake kumalizika mwaka 2018.

Mreno huyo mwenye miaka 31 amekua akihusishwa na kurudi kujiunga na timu yake ya zamani ya Manchester United, ambayo ilimuuza mwaka 2008 au Paris St-Germain, ya Ufaransa.

"Nataka kubakia hapa kwa miaka miwili zaidi, miaka miwili ninayozungumzia itanichukua mpaka mwisho wa maktaba wangu, "alinukuliwa mchezaji huyo.

Ronaldo alizungumza hayo wakati ya ghafla ya uchukuaji tuzo ya Pichichi, amabpo alishinda tuzo hiyo baada ya kuwa mfungaji bora mismu uliopita kwa kufunga mabao 48.

"Hii ni ligi bora duniani, japo kuwa pia nimecheza ligi ya England, ni ligi ya ushindani na inawachezaji wazuri."

Alhamisi, 4 Februari 2016

Jose Mourinho Huyoo OldTrafford

TRAFFORD

By Meshack Brighton

18:33TRANSFER ZONESHARE

0

Getty Images

Michael Owen alikaririwa akisema kuwa Mauricio Pochettino ndiye anayefaa kuwa kocha wa Manchester United lakini tetesi zinadai Jose Mourinho anakaribia kutua Old Trafford

Kuna taarifa zilizozagaa leo katika vyombo vya habari barani Ulaya kuwa kocha wa zamani wa Chelsea Jose Mourinho anakaribia kukubali na kusaini mkataba wa kuwa meneja wa Manchester United kwa msimu wa 2016/2017.

Mtandao wa habari wa Sky Sport Italia umethibitisha kuwepo kwa taarifa hizo.

Mreno huyo anayesemwa kuwa moja kati ya makocha bora na wenye mafanikio makubwa barani Ulaya amekuwa akihusishwa na mpango wa kujiunga na‘mashetani wekundu’ Manchester United tangu atimuliwe kibaruani na klabu ya Chelsea.

Taarifa zinaeleza zaidi kuwa Mourinho ameamua uamuzi huo wa kujiunga na Manchester United siku chache baada ya klabu ya Manchester City kutangaza ujio wa kocha wa Bayern Munich, Pep Guardiola.

Mourinho ambaye alikuwa na uhasimu mkubwa sana na Guardiola walipokuwa wote katika ligi kuu ya Hispania, La Liga kama atafanikiwa kujiunga na Manchester United basi watafanikiwa kurejesha uhasimu wao kwa mara nyingine tena.

Kwa sasa klabu ya Manchester United ipo nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi kuu Uingereza ikiwa na pointi 40 nyuma ya Arsenal iliyopo nafasi ya 4 kwa jumla ya pointi 45.

Jumamosi, 16 Januari 2016

KANISA LENYE UMBO LA KIATU LAJENGWA

ImageKanisa la kiatu

Kanisa la urefu wa mita 16 lililojengwa kwa kutumia vigae vya glasi linalofanana na viatu vyenye visigino virefu vinavyopendwa sana na wanawake limejengwa huko Taiwan kwa lengo la kuwavutia wanawake zaidi.

Likiwa limejengwa kwa kutumia vigae vya glasi takriban 320,kanisa hilo la rangi ya buluu lina upana wa mita 10 na limegharimu takriban dola 686,000.

Picha iliopigwa juu ya kanisa hilo pia imeonyesha ukubwa wa kanisa hilo pamoja na uzuri wa eneo lililojengwa.

Jumba hilo la kuabudu linatarajiwa kufunguliwa tarehe 8 mwezi Februari tayari kwa mwaka mpya wa Uchina.

Imagekanisa la kiatu Taiwan

Kiatu hicho kimetengezwa na maafisa wa baraza la miji kusini magharibi mwa pwani ,katika eneo moja la kitalii lenya umaarufu mkubwa huko Taiwan.

Lakini Pan Tsuei-ping,msimamizi wa ujenzi huo,ameiambia BBC kwamba kanisa hilo halitatumika kwa huduma za ibada za kila siku bali hafla za harusi.

''Katika mipango yetu,tunataka kulifanya eneo hili kuwa la kuvutia kimapenzi,kila msichana angepanda kutafakari atakapokuwa bibi harusi alisema'', Pan