Alhamisi, 24 Machi 2016

Mchezaji Adam Johson Afungwa jela miaka 6

Johnson alikuwa amechezea England mara 12

Mchezaji soka Adam Johnson amefungwa jela miaka sita kwa kushiriki mapenzi na msichana wa miaka 15.

Jaji Jonathan Rose amesema mchezaji huyo alitumia vibaya nafasi yake na kumsababishia mwathiriwa wake “madhara makubwa ya kisaikolojia”.

Jaji amemwambia Johnson, 28, kwamba alihsiriki ngono na msichana huyo akifahamu vyema kwamba alikuwa na umri wa chini ya miaka 16.

Imebainika pia kwamba polisi walipata kanda chafu za video zinazohusisha wanyama kwenye kompyuta mpakato ya Johnson.

Sunderland yavunja mkataba na Johnson

Hata hivyo, hatachukuliwa hatua kutokana na hilo.

ImageGetty

Mahakama ya Bradford iliambiwa kwamba mchezaji huyo alishiriki mapenzi na msichana huyo katika gari lake aina ya Range Rover Januari 2015.

Johnson alichezea timu ya taifa ya England mara 12. Alikuwa mchezaji wa klabu ya Sunderland.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni