Jumatatu, 8 Februari 2016

Makamishna Wa Uchaguzi ZEC Wapinga Uchaguzi Kurudiwa

uchaguzi Z’bar

 0

 0

 0

 0

 0

 0

 0

 

Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Ayoub Bakari Hamad akizungumza na waandishi Dar es Salaam jana kuhusu uchaguzi wa marudio visiwani humo. Kushoto ni mjumbe mwenzake, Nassor Khamis Mohammed. Picha na Salim Shao 

Kwa ufupi

Wajumbe hao wa chombo hicho cha uchaguzi pia wamesema hoja ya kupanga tarehe mpya ya uchaguzi iliyopendekezwa na mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha ilipingwa na wajumbe watatu na kuungwa mkono na wengine watatu.

By Raymond Kaminyoge, Mwananchi

Dar es Salaam. Makamishna wawili wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) wamejitokeza hadharani na kutangaza kupinga kurudiwa kwa uchaguzi wa rais, wawakilishi na madiwani, uamuzi wa kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, 2015 uliofanywa na mwenyekiti badala ya tume kinyume na sheria.

Wajumbe hao wa chombo hicho cha uchaguzi pia wamesema hoja ya kupanga tarehe mpya ya uchaguzi iliyopendekezwa na mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha ilipingwa na wajumbe watatu na kuungwa mkono na wengine watatu.

Makamishna hao, Nassor Khamis Mohamed na Ayoub Bakar Hamad walisema hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kwamba uchaguzi uliofanyika Zanzibar hautafutika kwa kuwa ulikuwa halali kikatiba.

Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salum Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi huo Oktoba 28, akisema kulikuwapo na ukiukwaji wa sheria na kanuni za uchaguzi na miezi miwili baadaye aliitangaza Machi 20 kuwa tarehe mpya ya kupiga kura.

Uchaguzi huo ulifutwa siku ambayo mshindi wa kiti cha urais alitakiwa atangazwe, huku matokeo ya majimbo 31 yakiwa yameshatangazwa na kura katika majimbo mengine tisa zikiwa zimeshahesabiwa. Pia, washindi wa nafasi za uwakilishi na udiwani walishatangazwa na kupewa hati za ushindi.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Nassor aliwataka wajumbe wenzake wa ZEC kutounga mkono uchaguzi wa marudio ili wasiwe sehemu historia mbaya ya nchi hiyo.

Alisema kifungu cha 119 (10) cha Katiba ya Zanzibar hakitoi nafasi kwa mwenyekiti peke yake kufanya uamuzi wa kufuta matokeo kwa jina la tume.

“Uamuzi mkubwa uliofanywa na mwenyekiti hauwezi kuchukuliwa kuwa uamuzi wa Tume na kurudia uchaguzi ni kuiweka nchi katika majaribu,” alisema.

Nassor alisema uchaguzi wa Zanzibar ulishakamilika katika ngazi za uwakilishi na udiwani huku wateule katika nafasi hizo wakikabidhiwa vyeti vyao kuthibitisha ushindi wao.

“Hakuna chombo chochote kinachoweza kubatilisha uchaguzi isipokuwa Mahakama Kuu baada ya kusikiliza shauri. Hao ndio ambao wametajwa kwenye sheria ya uchaguzi,” alisema.

Alisema uchaguzi wa rais wa Zanzibar haukulalamikiwa na mgombea yoyote kati ya 14 waliowania nafasi hiyo.

Nassor alisema yeye na wenzake wameendelea kuwepo kwenye tume hiyo ili kutoa ushauri kwa wenzao na pia kujua kinachoendelea na kuwafahamisha wananchi.

“Kwa hali ya Zanzibar ilivyo sasa anahitajika mpatanishi wa kimataifa ambaye ataziweka pande mbili za vyama vya siasa zinazotofautiana kisiasa katika meza ili kufikia suluhu,” alisema.

Kwa upande wake, Ayoub alisema Jecha anatakiwa kujipima, afanye uamuzi mgumu ili kuiepusha nchi kuingia katika vurugu.

Alisema kama uchaguzi huo ukifanyika, utatoa viongozi batili kwa sababu uchaguzi halali Zanzibar ulishafanyika.

Nassor alidai kuwa siku mbili baada ya kufuta matokeo ya uchaguzi Zanzibar, Jecha aliitisha kikao na kuomba wajumbe waunge mkono uamuzi huo, lakini nusu ya wajumbe walimuunga mkono na wengine walipinga.

Alisema Januari 21, mwaka huu tume ilikuwa na kikao kingine ili kujadili tarehe ya uchaguzi wa marudio.

“Baadhi ya wajumbe waliamua kuwa Machi 20, 2016 iwe ndiyo siku ya uchaguzi na wengine walipinga uchaguzi wakisema ufutaji wa matokeo ulikuwa batili kikatiba na kisheria,” alisema.

Alisema wakati Rais John Magufuli anachukua hatua nzito kuzuia matumizi mabaya ya fedha za umma, nchi yenye uchumi mdogo kama Zanzibar inatumia zaidi ya Sh7 bilioni kufanya uchaguzi wa marudio.

Jumamosi, 6 Februari 2016

Alhamisi, 4 Februari 2016

Jose Mourinho Huyoo OldTrafford

TRAFFORD

By Meshack Brighton

18:33TRANSFER ZONESHARE

0

Getty Images

Michael Owen alikaririwa akisema kuwa Mauricio Pochettino ndiye anayefaa kuwa kocha wa Manchester United lakini tetesi zinadai Jose Mourinho anakaribia kutua Old Trafford

Kuna taarifa zilizozagaa leo katika vyombo vya habari barani Ulaya kuwa kocha wa zamani wa Chelsea Jose Mourinho anakaribia kukubali na kusaini mkataba wa kuwa meneja wa Manchester United kwa msimu wa 2016/2017.

Mtandao wa habari wa Sky Sport Italia umethibitisha kuwepo kwa taarifa hizo.

Mreno huyo anayesemwa kuwa moja kati ya makocha bora na wenye mafanikio makubwa barani Ulaya amekuwa akihusishwa na mpango wa kujiunga na‘mashetani wekundu’ Manchester United tangu atimuliwe kibaruani na klabu ya Chelsea.

Taarifa zinaeleza zaidi kuwa Mourinho ameamua uamuzi huo wa kujiunga na Manchester United siku chache baada ya klabu ya Manchester City kutangaza ujio wa kocha wa Bayern Munich, Pep Guardiola.

Mourinho ambaye alikuwa na uhasimu mkubwa sana na Guardiola walipokuwa wote katika ligi kuu ya Hispania, La Liga kama atafanikiwa kujiunga na Manchester United basi watafanikiwa kurejesha uhasimu wao kwa mara nyingine tena.

Kwa sasa klabu ya Manchester United ipo nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi kuu Uingereza ikiwa na pointi 40 nyuma ya Arsenal iliyopo nafasi ya 4 kwa jumla ya pointi 45.

Arsene Wenger Amekubali Yaishe Kuhusu Ubingwa EPL

ARSENE WENGER ASALIMU AMRI ARSENAL

By Meshack Brighton

04:15PREMIER LEAGUESHARE

0

Getty Images

Arsene Wenger amekiri ni za haki na za kweli hukumu za EPL baada ya kulazimishwa sare tasa na Southampton Emirates na tumaini la ubingwa halipo tena

Kama ilikuwa imepangwa vile, wameshindwa kufunga mechi ya tatu mfululizo katika mechi nyingine ya Ligi Kuu ya Barclays na sare ya nyumbani ya 0-0 dhidi ya Southampton imeitupa Arsenal mbali kabisa katika mbio za ubingwa.

Arsenal wana pengo la pointi tano kutoka kwa vinara wa ligi Leicester na pointi tatu nyuma ya Manchester City wakikaribia kufikiwa na Tottenham wanaoshika nafasi ya nne.

Je! hali ni ile ile ya siku zote na hadithi zile zile za Profesa Wenger?

Arsene Wenger amekubali kuwa klabu yake ipo kwenye wakati mgumu katika mbio za ubingwa wa Ligi ya Uingereza kwa sasa.

Katika mahojiano na Daily Mail Arsene Wenger alinukuliwa akisema maneno haya kufuatia mwendo mbovu wa timu yake katika mechi tatu mfululizo.

“Tutaona mwisho wa msimu huu. Ni mapema sana kusema chochote”.

“Ni dhahiri tumekuwa na msimu mbaya hasa kuanzia ile mechi ya kwanza dhidi ya Liverpool na ile mechi dhidi ya Stoke ambayo kimsingi tumekuwa na tofauti kubwa sana katika michezo yetu miwili”, alisema Wenger.

 Pia kuhusu usajili wa mshambuliaji bora katika umaliziaji Arsene Wenger amekuwa akijitetea mara kwa mara na kusema kuwa hakuna washambuliaji bora sokoni kwa sasa ambao wanaweza kuimarisha safu aliyo nayo.

Amesema washambuliaji hawatafutwi mtaani bali kila mshambuliaji mkubwa yupo kwenye timu yake na ana mkataba.

"Huwezi tu kupita mtaani ukaanza kutafuta mshambuliaji."

"Wala huwezi kupata mshambuliaji atakayekwambia nipo hapa njoo unisajili."

Hayo ndiyo maneno ya Wenger, ni dhahiri ameona maji yamefika shingoni na hakuna ujanja anaweza kufanya.

Mambo Matano ambao hujui kuhusu Teknolojia

Habari tano za teknolojia ambazo hazifai kukupita

3 Februari 2016

Mshirikishe mwenzako

Teknolojia hubadilika mara kwa mara na kila siku kuna mambo mapya yanayovumbuliwa na mitindo pia kubadilika.

Hapa, kuna makala tano kuhusu teknolojia ambazo hazifai kukupita.

1. Li-fi ina kasi mara 100 zaidi ya Wi-fi

Teknolojia mpya ya kutuma data ijulikanayo kama Li-fi imefanyiwa majaribio.

Li-fi ina uwezo wa kumfanya mtumiaji kupata huduma ya mtandao mara 100 zaidi ya Wi-Fi na hutoa kasi ya hadi Gigabait moja kwa kila sekunde. Soma zaidi hapa: Li-fi ina kasi mara 100 zaidi ya Wi-fi

ImageTHINKSTOCK

2. Choo kinachojifungua na kujiosha

Choo cha kisasa ambacho kina uwezo wa kujifungua unapokaribia na pia kujiosha, ni moja ya vitu vinavyoonyeshwa katika maonyesho ya kimataifa ya teknolojia mpya za bidhaa za elektroniki Las Vegas.

Choo hicho, kilichopewa jina Neorest, pia humsafisha anayekitumia kwa kifaa kinachotoa maji moto na hewa mtu akiwa ameketi. Soma zaidi hapa: Choo kinachojifungua na kujiosha

ImageToto

3. Mercedes yazindua lori linalojiendesha

Mwanzo ilikuwa ni magari madogo sasa kampuni ya kutengeneza magari ya kifahari Daimler Mercedes-Benz imezindua lori linalojiendesha lenyewe!

Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo yenye asili yake nchini Ujerumani,Wolfgang Bernhard alibofya kidude na mara lori likachukua usukani na kuenda lenyewe pasi na kusababisha ajali ya aina yeyote. Soma zaidi hapa: Mercedes yazindua lori linalojiendesha

4. Je una simu ya Android? Soma utafiti huu

Simu za kisasa zinazotumia mfumo wa Android zinaweza kufuatiliwa kwa urahisi sana.

Uchunguzi umebaini kuwa simu zinazotumia mfumo huo zinaweza kufuatiliwa kwa urahisi mno pasi na kutumia kifaa cha GPS yake. Soma zaidi:Je una simu ya Android?

ImageGetty

5. Samsung yakiri TV zake zinanasa sauti

Samsung imewaonya wateja wake kuhusu kutojadili mambo yao ya kibinafsi mbele ya televisheni zao.

Onyo hilo ni kwa wale watazamaji ambao hudhibiti televisheni zao kwa kutumia sauti.

Baadhi ya runinga hizo za kisasa husikiliza mambo ambayo wanasema na zinaweza kuwasilisha ujumbe kwa Samsung au mashirika yanayohusiana na Samsung kibiashara. Soma zaidi hapa:Samsung yakiri TV zake zinanasa sauti

Nuh Mziwanda Amuomba Shilole Msamaha kwa Mara nyingine tena

Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’.

Musa Mateja, AMANI
STAA wa Wimbo wa Msondo Ngoma, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, anasemekana amemwangukia kwa mara nyingine aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kumtaka warudiane.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, Mbongo Fleva huyo amekuwa katika wakati mgumu tangu alipoachana na Shilole hivyo kulazimika kumpigia simu na kumwandikia ujumbe wa maneno akimuomba amsamehe na warejeshe penzi lao kama ilivyokuwa zamani.

“Ndugu yangu nikikwambia kuwa, Nuh maji yamemfika shingoni basi huna haja ya kuuliza mara mbili namna yalivyomfika kwani, juzikati nilikuwa naongea na Shilole akalalamika kwamba, jamaa huyo ameanza tabia ya kumpigiapigia simu akimwomba warudiane jambo ambalo Shilole analitolea nje,” kilisema chanzo hicho.

Akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole.

Baada ya kupenyezewa ubuyu huo, paparazi wetu alimtafuta Shilole kwa nia njema ya kutaka kujua ukweli wa madai hayo ambapo alisema ishu hiyo ipo ila hawezi kuanika wazi.

“Suala la Nuh kwa sasa sitaki kuendelea kuongea kwani nitakuwa nampigia debe mtu na kazi hiyo niliifanya sana. Unachotakiwa kujua kutoka kwangu ni kwamba mimi naendelea kupigania maisha tu ili niweze kusonga mbele na hapa nipo kipesa zaidi hivyo sina tena muda wa kuendelea kumpa nafasi bwana wa aina yeyote kwani hapo nyuma maisha yangu yalirudi nyuma hatua nyingi sana,” alisema Shilole.STAA wa Wimbo wa Msondo Ngoma, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, anasemekana amemwangukia kwa mara nyingine aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kumtaka warudiane.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, Mbongo Fleva huyo amekuwa katika wakati mgumu tangu alipoachana na Shilole hivyo kulazimika kumpigia simu na kumwandikia ujumbe wa maneno akimuomba amsamehe na warejeshe penzi lao kama ilivyokuwa zamani.

“Ndugu yangu nikikwambia kuwa, Nuh maji yamemfika shingoni basi huna haja ya kuuliza mara mbili namna yalivyomfika kwani, juzikati nilikuwa naongea na Shilole akalalamika kwamba, jamaa huyo ameanza tabia ya kumpigiapigia simu akimwomba warudiane jambo ambalo Shilole analitolea nje,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupenyezewa ubuyu huo, paparazi wetu alimtafuta Shilole kwa nia njema ya kutaka kujua ukweli wa madai hayo ambapo alisema ishu hiyo ipo ila hawezi kuanika wazi.

“Suala la Nuh kwa sasa sitaki kuendelea kuongea kwani nitakuwa nampigia debe mtu na kazi hiyo niliifanya sana.

Unachotakiwa kujua kutoka kwangu ni kwamba mimi naendelea kupigania maisha tu ili niweze kusonga mbele na hapa nipo kipesa zaidi hivyo sina tena muda wa kuendelea kumpa nafasi bwana wa aina yeyote kwani hapo nyuma maisha yangu yalirudi nyuma hatua nyingi sana,” alisema Shilole.

Jumatano, 3 Februari 2016

Kampuni Ya GOOGLE Imeizidi Thamani Kampuni Ya APPLE

Kampuni ya Google yaizidi Apple kwa thamani

2 Februari 2016

Mshirikishe mwenzako

ImageGettyImageGoogle imenufaika sana kutokana na matangazo kwenye simu

Kampuni ya Alphabet, inayomiliki Google, imeipita Apple na kuwa kampuni yenye thamani kubwa zaidi duniani.

Kwa mujibu wa ripoti ya mapato ya karibuni zaidi ya kampuni hiyo, faida yake ilifikia $4.9bn (£3.4bn) kwa robo ya tatu ya mwaka, ikipanda kutoka $4.7bn mwaka jana.

Tangazo hilo limesababisha bei ya hisa zake kupanda 9%.

Hii ina maana kwamba Alphabet sasa ina thamani ya $568bn, ikilinganishwa na Apple, ambayo thamani yake ni $535bn.

Hii ni mara ya kwanza kwa Alphabet kutenganisha mapato ya biashara ya Google, ambayo hujumuisha kisakuzi na YouTube, kutoka kwa biashara yake ya "Other Bets" ambayo hujumuisha miradi ya uvumbuzi kama vile magari ya kujiendesha na vipute vya kusambaza huduma za mtandao wa intaneti.

Kwa mwaka, Alphabet ilipata $16.3bn lakini takwimu zinaonyesha biashara yake ya "Other Bets" ilipoteza $3.6bn kipindi hicho, huku mapato ya jumla ya biashara ya Google yakipanda hadi $23.4bn, as kutokana na kuongezeka kwa matangazo mtandaoni.

"Inaonekana Google imeendelea kufanikiwa katika kufaidi kutoka kwa matangazo kwenye simu,” amesema Neil Doshi, meneja mkurugenzi wa utafiti katika kampuni ya Mizuho Securities.

"Miaka miwili au mitatu iliyopita, sekta ya simu ilitatiza sana Google. Kulikuwa na wasiwasi kwamba ingeathiri biashara zilizotegemea kompyuta, lakini huku simu sikianza kutumiwa sana kuchakura mtandaoni, matangazo kwenye simu yanakaribia yale ya kompyuta za kawaida kwa thamani.”

Uganda Wazindua Basi Linalotumia Nishati ya Jua


2 Februari 2016

Mshirikishe mwenzako

ImageBasi linalotumia umeme wa jua

Basi linalotumia umeme wa nguvu za jua ambalo limedaiwa na watengezaji wake nchini Uganda kuwa la kwanza barani Afrika limeendeshwa hadharani.

Basi hilo la kielektroniki aina ya Kayoola linalomilikiwa na kampuni ya Kiira Motors lilionyeshwa katika uwanja wa Uganda mjini Kampala.

Mojawapo ya betri zake zinaweza kuwekwa chaji na vibamba vya umeme wa jua katika paa la nyumba ambavyo huongeza kasi ya gari hilo hadi kilomita 80 kwa saa.

Watengezaji wake sasa wanalenga kuwavutia wateja wataolitengeza basi hilo ili kuvutia soko kubwa la magari duniani.

Mkurugenzi mkuu wa Kiira Motors Paul Isaac Musasizi ameiambia BBC kwamba amefurahishwa na jaribio la gari hilo lilipoendeshwa.

Raia wamefurahishwa na wazo kwamba Uganda ina uwezo wa kutengeza mfano kama huu na bw. Musasizi anasema kwamba angependelea kulisaidia taifa hilo kushindana na kampuni nyengine za magari katika eneo hili.

Pia anatumai kwamba hatua hiyo itabuni ajira zifikiazo 7000 kufikia mwaka 2018.Hatahivyo mradi huo hauwezi kuanza bila ya usaidizi wa kampuni zinazotengeza vifaa vya magari.

ImageBasi linalotumia umeme wa jua

Lengo ni kwamba kufikia 2039,kampuni hiyo itakuwa na uwezo wa kutengeza vifaa vya magari na kuviunganisha nchini Uganda bila kutegemea kampuni nyengine .

Basi hilo lenye viti 35 linalenga kufanya kazi katika miji midogo badala ya mji mkuu kutokana na masharti ya umbali linakoweza kusafiri.

Iwapo mabasi hayo yatazalishwa kwa wingi,kila basi litagharimu kiasi cha dola 58,000 ambacho bw,Musaizi anasema ni bei nzuri katika soko lenye ushindani mkubwa.

Kampuni ya Kiira Motors ilianzishwa kutokana na mradi uliofanyika katika chuo kikuu cha Makerere,ambacho ni mmoja wa mmiliki wa hisa katika kampuni hiyo na pia kimenufaika na ufadhili kutoka kwa hazina ya fedha ya serikali

Samatta Ameiokoa Simba

Samatta aikomboa Simba, aijengea uwanja

SIMBA sasa wamekaa mkao wa kula, kwani mwaka huu ni wa neema kwao. Kwanza watapata mgawo wa

Mbwana Samatta     

ADVERTISEMENT

SIMBA sasa wamekaa mkao wa kula, kwani mwaka huu ni wa neema kwao. Kwanza watapata mgawo wa asilimia 20 za mauzo ya straika wao wa zamani, Mbwana Samatta ambaye ameuzwa katika klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji akitokea TP Mazembe, pili wanasubiri kulipwa Dola 300,000 zaidi ya Sh 600 milioni ambazo wanaidai Etoile due Sahel ya Tunisia.

Katika mkataba wa Mazembe walipokuwa wanamnunua mchezaji huyo akitokea Simba uliwataka kuwapa Simba asilimia hizo watakapomuuza klabu nyingine jambo ambalo limetimia na wanatarajia kupokea Sh 349 milioni kutoka kwenye mauzo ya Dola 800,000 ambazo mmiliki wa Mazembe, Moise Katumbi amepewa na Genk huku Samatta akikunja fedha ndefu.

Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) liliiamuru Etoile kuilipa Simba ndani ya siku 60 ambazo zinakaribia kumalizika na Simba wamegoma kulipwa nusu nusu, wanataka pesa yao ilipwe kwa wakati mmoja na Etoile wakishindwa kuilipa Simba watakumbana na adhabu ya kushushwa daraja. Hivyo pesa hizo zikilipwa na zile za Samatta basi tatizo la ukata kwao litapungua.

Etoile walimnunua Emmanuel Okwi lakini hawakulipa hata shilingi na baadaye kuachana naye na Simba kulazimika kufungua kesi hiyo ya madai.

Rais wa Simba, Evans Aveva amesema kuwa kwasasa wanasubiri kupata mgawo wao huo na wamepanga pesa hizo kuzipeleka kwenye ujenzi wa uwanja wao uliopo Bunju B ambao utaanza kujengwa hivi karibuni. Kwa makadirio uwanja wa mazoezi na uzio wa nyavu unaweza kutumia Sh 150 milioni hivyo pesa hiyo itatosha kukamilisha ujenzi huo.

“Tunasubiri meneja wa Samatta arudi maana amekwenda Lubumbashi, ndipo tujue mgawo wetu tunapataje, ila tumepanga kuipeleka pesa hiyo kwenye ujenzi wa uwanja mzuri kabisa, fedha za Okwi bado hawajatulipa tunasubiri, muda waliopewa haujaisha, hatutaki kulipwa nusu tunahitaji fedha,’’ alisema Aveva.     

Bajeti Mpya Ya Serikali hii hapa


=

WEDNESDAY, FEBRUARY 3, 2016

Funga mkanda yawakuna wasomi

 0

 0

 0

 0

 0

 0

 0

 

 

Kwa ufupi

Katika mwongozo huo, Dk Mpango aliainisha mambo kadhaa ambayo ni vipaumbele vya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2016/17 na kutaja mbinu za ukusanyaji mapato, kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza mapato ya kodi na kupunguza matumizi ya Serikali.

By Florence Majani, Mwananchi fmajani@mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mpango wa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/ 2017 uliotolewa juzi na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango katika hotuba yake umepongezwa na wachumi huku wakiwa na wasiwasi kuhusu utekelezaji wake.

Katika mwongozo huo, Dk Mpango aliainisha mambo kadhaa ambayo ni vipaumbele vya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2016/17 na kutaja mbinu za ukusanyaji mapato, kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza mapato ya kodi na kupunguza matumizi ya Serikali.

Mengine ni kuimarisha viashiria vya uchumi na maendeleo, marejesho ya kodi, kupunguza gharama, kukuza pato halisi la Taifa na kupunguza nakisi ya Serikali kwenye misaada ya nje kwa zaidi ya asilimia tatu.

Kuimarisha mapato ya ndani

Katika hotuba yake, Dk Mpango alisema shabaha ya bajeti ya mwaka 2016/17 inalenga kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri kufikia asilimia 14.8 ya Pato la Taifa. Alisema mapato hayo yanatakiwa yafikie asilimia 15.3 mwaka wa fedha 2017/18 na asilimia 16.3 ifikapo 2019/20.

Ukusanyaji wa mapato

Katika ukusanyaji wa mapato ya kodi ili yafikie asilimia 13.2 ya Pato la Taifa kwa mwaka 2017/18 na asilimia 13.5 mwaka 2019/20, Dk Mpango alisema Serikali imefuta usimamiaji wa mapato unaofanywa na taasisi za Serikali na badala yake mapato hayo yatakusanywa na Wizara ya Fedha na Mipango.

Maeneo mengine ni kukusanya kodi za majengo, kurasimisha biashara ambazo hazijarasimishwa na kusimamia upatikanaji wa matumizi sahihi ya mashine ya EFD.

Kadhalika, hotuba hiyo ilisisitiza kupitiwa upya mikataba iliyopewa misamaha ya kodi.

Katika kipindi cha 2016/17 bajeti hiyo ililenga kukusanya jumla ya Sh14.1 bilioni kutoka kwenye vyanzo vya ndani ambayo ni asilimia 13.2 ya pato la ndani. Hiyo ikiwa ni ongezeko la asilimia 15.

Pato la Taifa na mfumuko wa bei

Aliitaka shabaha kuu kuwa ni kukuza pato halisi la Taifa kutoka asilimia saba mwaka 2015 hadi asilimia 7.2 kwa 2016 na kufikia asilimia nane 2017.

Mwongozo huo ulilenga pia kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha unabaki kwenye tarakimu moja na kufikia asilimia sita Juni 2016 na kubaki kati ya asilimia tano na nane katika kipindi cha muda wa kati.

Kupunguza matumizi

Waziri alisema Serikali ina mpango wa kupunguza matumizi yake kutoka asilimia 23.9 ya Pato la Taifa mwaka 2015/16 hadi asilimia 21.5 mwaka 2016/17.

Pia alitaka mashirika ya umma; Tanesco, Tazara, Shirika la Reli (TRL) Shirika la Ndege (ATCL) na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (Rahco), yajitegemee na kutengeneza faida badala ya kutegemea ruzuku ya Serikali.

Bajeti ya Serikali

Dk Mpango alisema bajeti hiyo inatarajia kupunguza nakisi ya Bajeti ya Serikali kwenye misaada ya nje kutoka asilimia 4.2 mwaka 2015/16 hadi chini ya asilimia 3.0.

Jumla ya Sh22, 991. 5 bilioni zinatarajiwa kukusanywa. Kati ya hizo, mapato ya ndani na ya halmashauri yataongezeka na kufikia Sh15,801 bilioni sawa na asilimia 69.7 ikilinganishwa na asilimia 62.2 ya 2015/16.

Katika jumla hiyo, mapato yasiyo ya kodi na mapato kutoka vyanzo vya halmashauri yatakuwa Sh584 bilioni, pia Serikali itakopa kiasi cha Sh1,782 bilioni kutoka vyanzo vya nje vyenye masharti ya kibiashara, mikopo ya ndani Sh3,300 bilioni na wadau wa kimaendeleo wanatarajiwa kuchangia Sh2,107 bilioni katika kipindi hicho.

Changamoto za nusu ya 2015/16

Licha ya kutoa shabaha ya bajeti ya mwaka 2016/17, Dk Mpango alieleza changamoto zilizoonekana kwenye bajeti ya nusu mwaka ya 2015/16 kuwa ni ukwepaji kodi kwa wafanyabiashara wasio waadilifu, mwitikio hasi kwenye matumizi ya EFD, kuongezeka kwa matumizi ya Serikali kusikowiana na hali halisi ya mapato na mazingira magumu ya ukusanyaji wa kodi katika sekta zisizo rasmi.

Wachumi wazungumzia mwongozo

Akizungumzia mkakati wa Serikali kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, Profesa wa Chuo Kikuu cha Ruaha, Gaudence Mpangala alipongeza mpango huo akisema katika Awamu ya Nne, Serikali ilikithiri kwa kuwa na matumizi mabaya ya fedha.

“Dk Mpango amefanya vyema kuweka hilo kwenye mwongozo. Kwa mfano, wabunge wasifanye sherehe zisizo za lazima na kupunguza safari za nje, yote hiyo ni azma ya kubana matumizi. Hilo tunalipongeza,” alisema.

Alisema hata Uchaguzi Mkuu ulikuwa na matumizi makubwa yasiyo ya lazima kwani hakukuwa na haja ya kununua magari ya polisi 770 wakati wa uchaguzi.

Kuhusu mashirika ya umma, Profesa Mpangala alisema yakifanya kazi kwa ufanisi yanaweza kujiendesha lakini kikwazo ni ufisadi na rushwa.

“Lakini suala si haya mashirika kujitegemea tu, bali kuweka mikakati dhabiti na kuondoa vikwazo vinavyofanya yasiendelee,” alisema.

Kuhusu mfumuko wa bei na ukusanyaji wa mapato, mchumi na mtafiti wa maendeleo wa Repoa, Profesa Samwel Wangwe alisema kwa kuwa uongozi wa sasa unaonekana makini, malengo hayo yatawezekana.

“Uongozi wa sasa si holela holela, watekelezaji wamefanya kazi yao. Kule kubana matumizi ni sawasawa ili fedha zihudumie watu na si watumishi,” alisema.

Mhadhiri wa uchumi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Stephen Kirama alisema miongozo na shabaha iliyotolewa na Waziri wa Fedha ni ya kisomi lakini ina changamoto kadhaa. Alisema kumlazimisha mfanyabiashara kutumia mashine za EFD ni jambo la moja na kuzitumia ni jambo jingine. “Lakini je, watu watakubali kudai risiti?” alisema.

Aliongeza zaidi kuwa katika suala la ukusanyaji wa kodi atakutana na changamoto za kutambua, kuorodhesha, kurasimisha na namna gani watachukua mkakati wa kukusanya kodi.

Kuhusu kupunguza utegemezi wa fedha za wahisani katika bajeti hadi kufikia asilimia chini ya tatu, Meneja Utafiti na Uchambuzi wa Sera wa Hakielimu, Godfrey Bonaventure alisema ili kufanikisha hilo ni lazima Serikali ipanue wigo wa ukusanyaji mapato.

Alisema ni lazima bajeti iendane na matumizi kwa kuhakikisha inakusanya mapato kutoka vyanzo vikuu vya mapato.     

Jumatatu, 1 Februari 2016

Tambwe:Kiiza haniwezi


ADVERTISEMENT


HEBU piga picha. Upande huu wa Msimbazi kuna Hamis Kiiza, kule Jangwani kuna Amissi Tambwe ambao kazi yao ni kutupia tu mabao. Kwa ukali wao huo wa kufumania nyavu kweli kuna timu itakayopona?
Kiiza amefikisha mabao 12 mpaka sasa, baada ya juzi Jumamosi kufunga mabao mawili wakati Simba ikiizamisha African Sports kwa mabao 4-0, hivyo kubakisha bao moja tu kumfikia Tambwe mwenye mabao 13 akiongoza orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu Bara msimu huu.   
Licha ya kasi ya Mganda wa Simba, Tambwe amemwambia Kiiza kwamba kamwe hawezi kumpata kwenye uwaniaji wa Kiatu cha Dhahabu.
Straika huyo wa Yanga anayetokea Burundi aliliambia Mwanaspoti kuwa anafahamu Kiiza ni mzuri na anamfukuzia kwenye upachikaji wa mabao lakini mbio zake haziwezi kumpita kwani anaamini yeye ni mkali kuliko Kiiza.
“Kiiza hawezi kunipata, nitajitahidi kwa kila hali ili niwe mbele zaidi yake. Hii ligi ni ngumu na ina upinzani mkubwa, tumepoteza mechi moja tunatakiwa kushinda mechi zote zilizobaki,” alisema Tambwe ambaye juzi Jumamosi alishindwa kuisaidia timu yake isiaibike Mkwakwani Tanga.
Yanga ilipoteza mechi yao ya kwanza katika msimu huu baada ya kucharazwa mabao 2-0 na Coastal Union katika pambano hilo lililovutia wengi.

Mzee Yusuph ft. Vanessa Mdee

Video mpya kutoka kwa mfalme Mzee Yusuph akimshirikisha mwanadada kutoka bongofleva,Vanessa Mdee

Ni ngoma nzuri kwakweli kwasababu kuna ladha mbili za muziki ndani ya hii ngoma kwahiyo naweza kusema ni ubunifu flani hivi ambao umefanyika.
Enjoy video hiyo 👆👆👆👆👆

Jumapili, 31 Januari 2016

Navy Kenzo Waachia Video yao Mpya

Video mpya kutoka kwa kundi la navy kenzo

Noma sana:Messi Kuanza kupokea bilioni 1.7 kwa wiki

KUFURU: Messi kuanza kupokea Sh 1.7 bilioni kwa wiki

SOKA linaelekea wapi? Hakuna anayejua. Lakini sasa imefika mahala ambapo mchezaji mmoja

ADVERTISEMENT

SOKA linaelekea wapi? Hakuna anayejua. Lakini sasa imefika mahala ambapo mchezaji mmoja anakaribia kulipwa dau la Sh1.7 bilioni kwa wiki kwa mujibu wa mshahara wake.

Staa wa Barcelona, Lionel Messi ambaye ni mmoja kati ya wachezaji wa kihistoria duniani anakaribia kulipwa dau la Pauni 583,000 kwa wiki ambazo ni sawa na Shilingi za Tanzania 1,778,120,000 kwa wiki na hivyo kuweka rekodi ya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani.

Dili hilo litamfanya Messi alipwe dau la Pauni 30 milioni kwa mwaka na hivyo kumfanya awe mchezaji anayelipwa zaidi kwa sasa wakati huu akiwa ameweka rekodi ya kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia mara nyingi zaidi. Mara tano.

Hilo litafanyika mwishoni mwa msimu katika kipindi cha majira ya joto wakati mkataba wa mchezaji huyo utakapoongezewa vipengele upya baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili ya nyongeza mwaka 2013 na mkataba huo unakoma mwaka 2018. Kwa mujibu wa kipengele kimoja cha nyaraka za mkataba wa Messi, imeandikwa kuwa mshahara wake utapandishwa mara mbili kuanzia mwanzoni mwa msimu 2016 bila ya kusaini mkataba mpya kutoka kwa huu wa sasa unaoisha 2018.

Kwa sasa Messi anaingiza dau la Pauni 17 milioni kwa mwaka lakini kwa mujibu wa mkataba huo, dau hilo linapaswa kwenda mpaka Pauni 29.8 milioni na hivyo kuzikata maini klabu mbili tajiri za Manchester City na PSG ambazo zinadaiwa kuwa katika nafasi ya kumtwaa Messi.

Dau la mshahara ambalo Manchester City walikuwa wamepanga kulitoa kwa Messi kwa sasa litakuwa pungufu kwa mshahara wa Pauni 200,000 kwa wiki lakini matumaini ya kumnasa Messi yanazidi kukatika zaidi baada ya kugundulika kuwa kama Barcelona ikiamua kumuuza staa huyo, basi suala hilo litakuja akiwa katika mshahara mpya.

ADVERTISEMENT

Kwa mujibu wa mkataba huo, Barcelona italazimika kulipa dau la Pauni 15 milioni kama fidia kwa Messi kama ikiamua kumuuza kabla ya nyongeza hiyo ya mshahara haijaanza kufanya kazi.

Licha ya dau hilo la mshahara, kwa mujibu wa Jarida la France Football la Mei 2015, Messi mwenye umri wa miaka 28 anadaiwa kukusanya kiasi cha Pauni 48 milioni kwa mwaka 2014 ukijumlisha na bonasi zake mbalimbali, mshahara na mikataba ya kibiashara.

Mauzo ya sura yake katika mikataba yake ya kibiashara kama Turkish Airlines, Fifa video Games na mingineyo yamemwongezea dau la Pauni 1.8 milioni kwa mwaka na hivyo kufikia idadi ya Pauni 21 milioni kwa mwaka.

Messi ambaye anakaribia kufikia rekodi ya staa wa zamani wa England, David Beckham ya kumaliza nafasi hiyo ya juu kwa utajiri kwa mwaka wa sita mfululizo, bado amemwacha mbali mpinzani wake wa karibu wa uwanjani, Cristano Ronaldo wa Real Madrid licha ya Ronaldo kuongeza mapato yake kwa wingi katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.

Ronaldo (31), aliongeza kiasi cha Pauni 11 milioni na hivyo kufikia dau la Pauni 40 milioni kwa mwaka wakati Neymar wa Barcelona ameongeza mapato yake kuanzia Pauni 21 milioni hadi 27 milioni.

Wachezaji tisa wana pato la zaidi ya Pauni 15 milioni kwa mwaka akiwemo nahodha wa PSG, Thiago Silva anayeingiza Pauni 20 milioni kwa mwaka huku staa wa timu yake, Zlatan Ibrahimovic akiingiza Pauni 15.8 milioni.

Jumamosi, 30 Januari 2016

Samatta Lazima Ang'are Pale Grenk

Kwa fowadi hii ya Genk? Samatta labda arogwe

KWA mwanetu Mbwana Samatta tunayemjua na kwa Genk hii aliyokwenda,  labda alogwe. Lakini hakuna

Camargo

ADVERTISEMENT

KWA mwanetu Mbwana Samatta tunayemjua na kwa Genk hii aliyokwenda,  labda alogwe. Lakini hakuna kitakachomzuia kuingia kwenye kikosi cha kwanza baada ya jana Ijumaa jioni kusaini mkataba wa miaka minne ambao unaanzia 2016-2020 mwaka ambao Rais John Magufuli atakuwa anatimiza miaka mitano ya kuongoza nchi.

Samatta ameikuta Genk ina mastraika saba kutoka Uturuki, Jamaica, Ugiriki, Georgia na wazawa wa Ubelgiji.

Huyo straika wa Uturuki anaitwa Enes Unal ni mchezaji wa Manchester City ya England ambaye ameletwa Genk kwa mkopo wa misimu miwili huu ni msimu wake wa kwanza na amepachika bao moja tu katika mechi zaidi ya 10 alizocheza.

 Huyo wa Georgia ni jamaa mmoja mtata sana uwanjani anaitwa Nikolaos Karelis anatumia guu la kushoto, mpaka sasa amefunga bao moja tu.

Sasa kuna mashine zao mbili wanazoziaminia ijapokuwa kiuhalisia umri umewatupa. Mmoja anaitwa Igor Alberto Camargo ana miaka 32, huyu jamaa amefunga mabao matano tu katika mechi zote 23 alizocheza.

Ni Mbrazili aliyepewa uraia wa Ubelgiji. Hao wangapi? Staa mwingine ni kibabu pia ana miaka 34 wanamuita Thomas Buffel ni pande fulani la mtu amefunga mabao matatu. Huyo wa Jamaica anaitwa Leon Bailey ni bwana mdogo kuliko hata Samatta, yeye ana mabao matatu.

Hao mafowadi wengine wala hata usitake kuwajua utakuwa unapoteza muda wako tu. Ila kwa jinsi Samatta alivyopania lazima mtu aende benchi.Sikia sasa mastraika saba wa Genk kwa ujumla wao katika mechi zote 23 walizocheza wamefunga mabao 12. Buffel na Camargo wamefunga mabao manane kati ya hayo. Ukiangalia takwimu hizo za mabao unapata jibu la kwanini Kocha Mbelgiji, Peter Maes alimtaka Samatta kwa nguvu zote kuokoa kibarua chake. Genk ipo katika nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi ikiwa pointi 32, huku AA Gent wakiongoza msimamo kwa pointi 49.

Kwenye timu hiyo kuna Wakongomani wanne ambao wamezaliwa Ubelgiji wana uraia wa nchi mbalimbali. Wakongomani hao ni Derick Katuku Tshimanga ambaye ni beki wa kushoto anayetumia mguu wa kulia mwenye kilo 68 ana miaka 27.

Mwingine ni Christian Kabasele ambaye ni bonge la beki anatumia guu la kulia na kwa sasa amepachika mabao mawili kwenye ligi. Kuna Mkongo Mwingine anaitwa Neesken Kebano ni kiungo ana mabao matatu msimu huu.

Kuna Mnigeria anaitwa Onyinye Ndidi ni beki fulani mjanja mjanja mwenye bao moja. Yule Mghana Bennard Kumordzi ni beki. Wachezaji hao wameshazoea mazingira kwenye kikosi hicho na huenda wakawa msaada mkubwa kwa Mbwana Samatta ambaye jana Ijumaa alitaraji kufanyiwa vipimo vya afya pamoja na TP Mazembe kumalizana na Genk.

TP Mazembe jana ilikuwa kwenye mishemishe za kumalizana na Genk na kupokea dau lao la zaidi ya Sh.1.8 bilioni ambapo Simba wanasubiri mgao wao kutoka hapo. Klabu ya Genk  baada ya kushiriki Ligi ya Mabingwa mwaka 2012 iliwauza kipa wa sasa wa Chelsea, Thibaut Courtois na  Kevin De Bruyne ambaye pia alienda Chelsea kabla ya kutua Man City. Ilimuuza pia Christian Benteke kwa Aston Villa, sasa yuko Liverpool.